Saturday , 18 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Mbunge ataka nafuu wanafunzi wanaochanganyikiwa mtihani kidato cha nne
ElimuHabari za Siasa

Mbunge ataka nafuu wanafunzi wanaochanganyikiwa mtihani kidato cha nne

Wanafunzi
Spread the love

 

MBUNGE Viti Maalumu, Sophia Mwakagenda, ameishauri Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, itumie matokeo ya nyuma ya wanafunzi katika kuamua ufaulu wa mtihani wa mwisho wa kidato cha nne, ili kuwasaidia wanaochanganyikiwa wakati wakifanya mitihani hiyo ya kuhitimu elimu ya sekondari. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mwakagenda ametoa ushauri huo leo Jumatano, tarehe 25 Mei 2022, katika kipindi cha maswali na majibu, bungeni jijini Dodoma.

“Hamuoni kwamba mtihani wa mwisho wa kidato cha nne mwanafunzi anapofanya wakati mwingine anaweza akawa amechanganyikiwa. Kwa nini wizara isiangalie matokeo ya nyuma jumlisha na yale ya mwisho tuweze kumhukumu kuendelea na maisha yake,” amesema Mwakagenda.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omary Kipanga, amesema katika upangaji wa matokeo ya mtihani wa kidadto cha nne, huchukua asilimia 30 ya maendeleo yake ya elimu katika kipindi cha miaka minne, kisha inajumlisha asilimia 70 ya matokeo ya mtihani wa mwisho.

“Naomba nimhakikishie mbunge kwamba mtihani wetu wa mwisho ule wa form four sio unaopelekea kuwa na matokeo ya mwisho. Mtihani wetu una maeneo mawili, asilimia 30 inakuwa kwenye maendeleo ya elimu. Asilimia 30 zinatoka kwenye maendeleo yake aliyofanya miaka minne,” amesema Kipanga ana kuongeza:

“Asilimia 70 zinazingatiwa kwenye ule mtihani wake wa mwisho iwapo kama amefanya vizuri kwenye maendeleo yake kutoka kidato cha kwanza mpaka cha nne. Ile asilimia 30 itambeba na kuchangia asilimia 70 ya matokeo yake. Hilo Serikali limezingatia na ndilo linaendelea mpaka sasa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Haya hapa majina walioteuliwa kugombea nafasi mbalimbali CHADEMA

Spread the loveCHAGUZI wa kanda za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)...

error: Content is protected !!