Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari Tanzania kufikisha ndege 16, ATCL yajitanua
HabariTangulizi

Tanzania kufikisha ndege 16, ATCL yajitanua

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema, hadi kufikia Februari 2022 Serikali imekwisha kulipa malipo ya awali ya ununuzi wa ndege mpya tano. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Majaliwa amesema hayo leo Jumatano, tarehe 6 Aprili 2022, wakati akiwasilisha Bajeti ya Ofisi yake kwa mwaka wa fedha 2022/23 Bungeni jijini Dodoma ya Sh.148.89 bilioni na Sh.132.7 bilioni kwa ajili ya Mfuko wa Bunge.

Amesema, Serikali katika mwaka 2021/2022 imeendelea kuliimarisha Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) ili liweze kutoa huduma bora ya usafiri wa anga ndani na nje ya Tanzania.

Majaliwa amesema, kati ya meli hizotano, ndege moja ni aina ya Boeing 787-8 Dreamliner; ndege mbili aina ya Boeing 737-9; ndege moja aina ya De Havilland Dash 8-Q400; na ndege moja ya mizigo aina ya Boeing 767-300F.

“Kukamilika kwa ununuzi wa ndege hizo, kutaiwezesha Serikali kuwa na jumla ya ndege mpya 16,” amesema Majaliwa

Majaliwa amesema, kutokana na kuendelea kuimarika kwa ATCL, hivi karibuni limefanikiwa kuanza safari katika vituo vya Arusha, Geita, na kurejesha safari za Mtwara na Songea.

Aidha, limerudisha safari za kikanda katika vituo vya Bujumbura, Entebbe, Harare, Lusaka na Hahaya pamoja na kuanzisha vituo vipya vitatu katika miji ya Lubumbashi, Nairobi na Ndola.

Vilevile, Shirika limefanikiwa kurejesha safari ya kimataifa kwenda Mumbai – India pamoja na kuanzisha safari za mizigo kuelekea Guangzhou – China.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Migogoro ya ndoa yaongezeka, Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveMIGOGORO ya ndoa na familia imeongezeka kwa asilimia 8.3  kutoka...

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Hatuoni faida ya demokrasia

Spread the loveMwenyekiti wa Chadema, Fremaan Mbowe amesema Tanzania haijanufaika na miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ataka wananchi wasiruhusu bakora za Magufuli

Spread the loveMwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Profesa Ibrahimu Lipumba...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mbunge Mwakasaka alitaka Jeshi la Polisi kutenda haki

Spread the loveEMMANUEL Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini (CCM), amelitaka Jeshi...

error: Content is protected !!