Tuesday , 21 May 2024
Home Habari Mchanganyiko THRDC yawanoa watetezi wa haki za binadamu Zanzibar
Habari Mchanganyiko

THRDC yawanoa watetezi wa haki za binadamu Zanzibar

Spread the love

MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umewapa mafunzo ya namna kufuatilia na kuripoti matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu, wadau kutoka Asasi za Kiraia (AZAKI), za Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Mafunzo hayo yameanza kutolewa leo Jumanne, tarehe 15 Machi 2022, katika Hoteli ya Golden Tulip, visiwani Zanzibar na kufunguliwa na Meya wa Jiji la Zanzibar, Mahmoud Musa.

Akifungua mafunzo hayo, Mussa amewataka washiriki hao zaidi ya 50, kuyatumia katika kutokomeza changamoto za ukatili wa kijinsia visiwani humo.

“Nawasihi muwe mabalozi wazuri kuhakikisha kwamba udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto, kuhakikisha tatizo hili linaondoka katika nchi yetu,”amesema Mussa.

Kwa upande wake Mratibu wa THRDC, Onesmo Olengurumwa, mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo juu ya namna ya kufuatilia, kuhifadhi na kutoa taarifa zinazogusa masuala ya udhalilishaji wa kijinsia hususan wanawake na watoto.

“Tunafahamu Zanzibar ina changamoto mbalimbali za haki za binadamu, hasa zinazogusa masuala ua udhalilishaji, mfano dawa za kulevya na mambo yanayohusu masuala ya haki za wanawake na watoto. Mafunzo haya yanawajengea uwezo wa kuyafuatilia na kuripoti,” amesema Olengurumwa.

Olengurumwa amesema kuwa, katika mafunzo hayo watapata nafasi ya kutoa maoni yao juu ya kutatua changamoto za kimahakama, kwa wataalamu wanaofanya mapitio ya changamoto hizo, pamoja na kujipanga katika kuweka mikakati ya kufanya kazi na Serikali pamoja na wadau wengine katika kutetea haki za binadamu.

Olengurumwa amesema kuwa, katika mafunzo hayo watapata nafasi ya kutoa maoni yao juu ya kutatua changamoto za kimahakama, kwa wataalamu wanaofanya mapitio ya changamoto hizo, pamoja na kujipanga katika kuweka mikakati ya kufanya kazi na Serikali pamoja na wadau wengine katika kutetea haki za binadamu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watumishi 25,039, taasisi 65 wahamia Dodoma

Spread the loveSerikali imesema hadi sasa, jumla ya watumishi 25,039 kutoka Serikali...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yapata idhini kuwa wakala wa madalali wa DSE

Spread the loveBenki ya NMB imepata idhini kutoka Benki Kuu ya Tanzania...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Waziri aipongeza NBS kwa mafanikio

Spread the loveNaibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande amepongeza Ofisi ya Taifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Balozi Nchimbi aonya maofisa utumishi kuacha uonevu

Spread the loveKatibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel...

error: Content is protected !!