RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Dk. Nicolaus Shombe kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Kabla ya uteuzi huo, Dk. Shombe alikuwa Kamishna wa Mipango- Wizara ya Fedha na Mipango.
Dk. Shombe, anachukua nafasi ya Profesa Damian Gambagambi ambaye alifariki dunia Jumanne ya tarehe 20 Oktoba 2020, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam
Uteuzi huo, umeanza tarehe 29 Oktoba 2021.
Taarifa ya uteuzi wake, imetolewa jana Jumatatu, tarehe 1 Novemba 2021 na Jaffar Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.
Rais Samia amefanya uteuzi huo akiwa Glasgow nchini Scotland anakohudhulia mkutano wa 26 wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi (CPO26).
Mkutano huo, umeanza jana Jumatatu na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wakuu wa nchi na leo Jumanne, Rais Samia anatarajia kuhutubia mkutano huo.
Leave a comment