Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia afanya uteuzi akiwa Scotland
Habari Mchanganyiko

Rais Samia afanya uteuzi akiwa Scotland

Spread the love

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Dk. Nicolaus Shombe kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Shombe alikuwa Kamishna wa Mipango- Wizara ya Fedha na Mipango.

Dk. Shombe, anachukua nafasi ya Profesa Damian Gambagambi ambaye alifariki dunia Jumanne ya tarehe 20 Oktoba 2020, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam

Uteuzi huo, umeanza tarehe 29 Oktoba 2021.

Taarifa ya uteuzi wake, imetolewa jana Jumatatu, tarehe 1 Novemba 2021 na Jaffar Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Rais Samia amefanya uteuzi huo akiwa Glasgow nchini Scotland anakohudhulia mkutano wa 26 wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi (CPO26).

Mkutano huo, umeanza jana Jumatatu na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wakuu wa nchi na leo Jumanne, Rais Samia anatarajia kuhutubia mkutano huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!