Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Askari polisi 7 wa Tanzania walioingia Malawi watimuliwa
Habari Mchanganyiko

Askari polisi 7 wa Tanzania walioingia Malawi watimuliwa

Spread the love

 

ASKARI saba wa Jeshi la Polisi Tanzania wamefukuzwa kazi baada ya kuvuka mpaka na kuingia nchini Malawi kinyume cha utaratibu wa jeshi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Songwe … (endelea).

Askari hao ni wa Wilaya ya Ileje Mkoa wa Songwe ambao tarehe 15 Septemba 2021, wakiwa wamevalia sare za jeshi hilo waliingia Malawi wakidaiwa kufukuzia magendo.

Wakiwa huko, wananchi wa Malawi waliwavamia na kuanza kuwapiga na kuharibu gari la polisi.

https://youtu.be/cPCxiUNTdHk

Leo Jumanne, tarehe 21 Septemba 2021, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, ACP Janeth Magomi ametangaza kufukuzwa kazi askari hao kwa kuingia Malawi pasina kibali cha Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP).

Kamanda Janeth amewataja askari hao saba waliotimuliwa; ni PC Edward, PC Safari, PC Joseph, PC Hussein, WP Anastazia na PC Jumanne ambaye alikuwa dereva.

Amesema, askari hao wanaweza kufuata utaratibu na kukata rufaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

error: Content is protected !!