ASKARI saba wa Jeshi la Polisi Tanzania wamefukuzwa kazi baada ya kuvuka mpaka na kuingia nchini Malawi kinyume cha utaratibu wa jeshi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Songwe … (endelea).
Askari hao ni wa Wilaya ya Ileje Mkoa wa Songwe ambao tarehe 15 Septemba 2021, wakiwa wamevalia sare za jeshi hilo waliingia Malawi wakidaiwa kufukuzia magendo.
Wakiwa huko, wananchi wa Malawi waliwavamia na kuanza kuwapiga na kuharibu gari la polisi.
https://youtu.be/cPCxiUNTdHk
Leo Jumanne, tarehe 21 Septemba 2021, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, ACP Janeth Magomi ametangaza kufukuzwa kazi askari hao kwa kuingia Malawi pasina kibali cha Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP).
Kamanda Janeth amewataja askari hao saba waliotimuliwa; ni PC Edward, PC Safari, PC Joseph, PC Hussein, WP Anastazia na PC Jumanne ambaye alikuwa dereva.
Amesema, askari hao wanaweza kufuata utaratibu na kukata rufaa.
Leave a comment