Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Askari polisi 7 wa Tanzania walioingia Malawi watimuliwa
Habari Mchanganyiko

Askari polisi 7 wa Tanzania walioingia Malawi watimuliwa

Spread the love

 

ASKARI saba wa Jeshi la Polisi Tanzania wamefukuzwa kazi baada ya kuvuka mpaka na kuingia nchini Malawi kinyume cha utaratibu wa jeshi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Songwe … (endelea).

Askari hao ni wa Wilaya ya Ileje Mkoa wa Songwe ambao tarehe 15 Septemba 2021, wakiwa wamevalia sare za jeshi hilo waliingia Malawi wakidaiwa kufukuzia magendo.

Wakiwa huko, wananchi wa Malawi waliwavamia na kuanza kuwapiga na kuharibu gari la polisi.

https://youtu.be/cPCxiUNTdHk

Leo Jumanne, tarehe 21 Septemba 2021, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, ACP Janeth Magomi ametangaza kufukuzwa kazi askari hao kwa kuingia Malawi pasina kibali cha Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP).

Kamanda Janeth amewataja askari hao saba waliotimuliwa; ni PC Edward, PC Safari, PC Joseph, PC Hussein, WP Anastazia na PC Jumanne ambaye alikuwa dereva.

Amesema, askari hao wanaweza kufuata utaratibu na kukata rufaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!