Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Simbachawene : Serikali imewadhibiti  majambazi 
Habari Mchanganyiko

Simbachawene : Serikali imewadhibiti  majambazi 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), George Simbachawene
Spread the love

 

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, amesema Jeshi la Polisi limefanikiwa kudhibiti vitendo vya uhalifu wa kutumia silaha ‘ujambazi’ ulioibuka hivi karibuni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Simbachawene ametoa kauli hiyo jana tarehe 3 Julai 2021, akizungumza na wananchi wa Jimbo lake la Kibakwe, jijini Dodoma.

Simbachawene alisema, jeshi hilo limefanikiwa kuwanyamazisha kimyakimya majambazi katika maeneo mbalimbali nchini, baada ya hivi karibuni kuijaribu Serikali.

Simbachawene alisema baadhi ya matukio ya ujambazi yalitokea hivi karibuni, katika baadhi ya miji ya Dar es Salaam, Arusha na Mwanza.

Waziri huyo wa mambo ya ndani alisema, majambazi hao walinyamazishwa katika operesheni ya kwanza ya kupambana na majambazi, iliyofanyika hivi karibuni nchi nzima.

Huku akiwaonya wahalifu hao wasiendelee kuijaribu Serikali, kwa kuwa inaendelea kufanya operesheni ya awamu ya pili.

 “Wapo watu wengine wanafikiri uhalifu utawasaidia, kwa wale ambao wanavichwa vigumu wanaendelea kuichezea Serikali kwa kutokutaka kuacha uhalifu, kuacha ujambazi wa kutumia silaha, wanaopenda kubaka, wanaopenda kunyang’anya, wanaotumia pikipiki kupora,”

“Sisi tumeyaweka makosa hayo kama makosa makubwa, tukikukamata tunamalizana naye kimyakimya, wewe utajua kimyakimya tunamalizana kinamna gani,” alisema Simbachawene.

Simbachawene aliwataka Watanzania kufanya kazi halali, kwa kuwa fursa za kiuchumi zipo nyingi nchini, kuliko kufanya uhalifu ambao utawaletea matatizo.

“Nawaomba Watanzania na leo nazungumzia hapa Lufu, Jimbo la Kibakwe, Wilaya ya Mpwapwa, nataka kauli hii ifike nchi nzima, kwamba uhalifu sio dili,

Serikali ipo makini, tutadili na wahalifu wote mpaka tone la mwisho.

Acheni kufanya uhalifu, ukiwa mtu wa kupanga mambo yako utafanikiwa tu, lakini uhalifu hauwezi kukusaidia,” alisema Simbachawene.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

error: Content is protected !!