Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mbunge ahoji sababu ofisi za CCM kugeuzwa Mahakama
Habari Mchanganyiko

Mbunge ahoji sababu ofisi za CCM kugeuzwa Mahakama

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Geofrey Pinda
Spread the love

 

MBUNGE wa Kalambo mkoani Rukwa (CCM), Josephat Kandege, amehoji sababu za jengo la Chama cha Mapinduzi (CCM), kutumiwa na Mahakama ya Wilaya ya Kalambo, kuendesha shughuli zake, kitendo kinachokosesha chama hicho mapato. Anaripoti Jemima Samwel, DMC … (endelea).

Kandege amehoji hayo leo Jumatatu, tarehe 7 Juni 2021, katika kipindi cha maswali na majibu, bungeni jijini Dodoma.

“Mahakama ya Wilaya ya Kalambo sasa hivi wanatumia jengo la CCM na hivyo sisi kama CCM, tunaona wanatunyima mapato,” amesema Kandege.

Mbunge huyo wa Kalambo, ameihoji Serikali ina mpango gani kujenga jengo la mahakama ya wilaya hiyo.

“Je, Serikali iko tayari katika mpango wa kujenga mahakama ya wilaya, ili Wilaya ya Kalambo ikapewa kipaumbele kujenga mahakama ya kisasa, yenye kulingana na hadhi ya wilaya yetu?” amesema Kandege.

Wakati huo huo, Kandege ameiomba Serikali ipeleke watumishi wa mahakama hususan mahakimu, ili wananchi wapate huduma za kisheria.

Mbunge wa Kalambo mkoani Rukwa (CCM), Josephat Kandege

Akimjibu Kandege, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Geofrey Pinda, amesema Serikali ina mkakati wa kujenga majengo ya mahakama za wilaya nchi nzima na kuwa hadi kufikia 2026, wilaya zote zitakuwa na majengo hayo.

“Tunao mkakati kufikia 2025/26, nchi nzima katika makao makuu ya wilaya zote, zitakuwa na majengo ya mahakama. Na makao makuu ya tarafa zote nchini yatakuwa yamepata majengo, nimuombe mheshimiwa awe mvumilivu,” amesema Pinda.

Kuhusu uhaba wa watumishi wa mahakama, Pinda amesema Serikali inaifahamu changamoto hiyo, na kwamba itaongeza watumishi kadri itakavyowezekana.

“Kuhusu swali la kwanza linalohusu suala la watumishi na mahakimu, ni mpango wa mahakama kuongeza idadi ya mahakimu ili iweze kutosheleza, ingawa kwa kweli bado tatizo ni kubwa la watumishi katika sekta mbalimbali nchini,” amesema Pinda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!