Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko RC Dar aagiza usafi kila Jumamosi, Ma DC…
Habari Mchanganyiko

RC Dar aagiza usafi kila Jumamosi, Ma DC…

Spread the love

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Aboubakar Kunenge amewataka wakuu wa wilaya za jiji hilo (DC) kuhakikisha wanasimamia shughuli ya usafiri wa mazingira kila Jumamosi. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Kunenge amewataka wananchi wa Mkoa huo kuhakikisha kila Jumamosi kuanzia saa 12 hadi saa tatu asubuhi usafi unafanyika ili kujikinga na magonjwa ya mlipuko na kuliweka jiji kuwa safi.

Mkuu hiyo wa mkoa, ametoa maagizo hayo jana Jumanne tarehe 1 Desemba 2020 wakati alipokuwa anazungumzia shughuli ya usafi inayotarajia kufanyika Jumamosi ya 5 Desemba.

Alisema Mkoa umejipanga vizuri kuhakikisha magari ya kubeba taka yanakuwa ya kutosha kwenye kila maeneo.

Aidha RC Kunenge aliwataka wakuu wa wilaya za Jiji hilo za Kinondoni, Ilala, Ubungo, Temeke na Kigamboni kuhakikisha wanasimamia usafi maeneo yao na kuhakikisha suala la usafi linazingatiwa na kila mmoja.

Pamoja na hayo RC Kunenge alitoa wito kwa wananchi wa Mkoa huo kuhakikisha suala la usafi linakuwa sehemu ya maisha yao na sio kusubiri kushurutishwa na sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

error: Content is protected !!