Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Elisha wa TBC aagwa Dar, kuzikwa kesho  
Habari Mchanganyiko

Elisha wa TBC aagwa Dar, kuzikwa kesho  

Spread the love

MWILI wa Mwandishi wa Habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Elisha Elia (39), umeangwa jijini Dar es Salaam kisha kusafirishwa kwenda Tukuyu Mbeya kwa maziko kesho Jumanne tarehe 27 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). 

Elisha alifikwa na mauti Jumamosi iliyopita tarehe 24 Oktoba 2020 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akisumbuliwa na vidonda vya tumbo vilivyoanza kumsumbua mapema mwezi huu.

Mamia ya ndugu, jamaa na marafiki wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge wameshiriki kuaga mwili wa Elisha leo Jumatatu tarehe 26 Oktoba 2020 katika Kanisa la KKKT Usharika wa Segerea.

Akitoa salamu za Serikali, Kunenge amesema, Elisha amekuwa chuo kwa yale yote aliyoyafanya kwa taifa lale.

Elisha ameacha mjane na watoto wawili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari Mchanganyiko

Shahidi aeleza namna Nathwani alivyomjeruhi jirani yake

Spread the loveMSIMAMIZI wa Msikiti wa Wahindi Lohana aitwae, Ankit Dawda (32)...

error: Content is protected !!