Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Elisha wa TBC aagwa Dar, kuzikwa kesho  
Habari Mchanganyiko

Elisha wa TBC aagwa Dar, kuzikwa kesho  

Spread the love

MWILI wa Mwandishi wa Habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Elisha Elia (39), umeangwa jijini Dar es Salaam kisha kusafirishwa kwenda Tukuyu Mbeya kwa maziko kesho Jumanne tarehe 27 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). 

Elisha alifikwa na mauti Jumamosi iliyopita tarehe 24 Oktoba 2020 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akisumbuliwa na vidonda vya tumbo vilivyoanza kumsumbua mapema mwezi huu.

Mamia ya ndugu, jamaa na marafiki wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge wameshiriki kuaga mwili wa Elisha leo Jumatatu tarehe 26 Oktoba 2020 katika Kanisa la KKKT Usharika wa Segerea.

Akitoa salamu za Serikali, Kunenge amesema, Elisha amekuwa chuo kwa yale yote aliyoyafanya kwa taifa lale.

Elisha ameacha mjane na watoto wawili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!