Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Elisha wa TBC aagwa Dar, kuzikwa kesho  
Habari Mchanganyiko

Elisha wa TBC aagwa Dar, kuzikwa kesho  

Spread the love

MWILI wa Mwandishi wa Habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Elisha Elia (39), umeangwa jijini Dar es Salaam kisha kusafirishwa kwenda Tukuyu Mbeya kwa maziko kesho Jumanne tarehe 27 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). 

Elisha alifikwa na mauti Jumamosi iliyopita tarehe 24 Oktoba 2020 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akisumbuliwa na vidonda vya tumbo vilivyoanza kumsumbua mapema mwezi huu.

Mamia ya ndugu, jamaa na marafiki wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge wameshiriki kuaga mwili wa Elisha leo Jumatatu tarehe 26 Oktoba 2020 katika Kanisa la KKKT Usharika wa Segerea.

Akitoa salamu za Serikali, Kunenge amesema, Elisha amekuwa chuo kwa yale yote aliyoyafanya kwa taifa lale.

Elisha ameacha mjane na watoto wawili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!