Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Lema, Gambo wakutana mgahawani
Tangulizi

Lema, Gambo wakutana mgahawani

Spread the love

WAGOMBEA Ubunge Arusha Mjini, Mrisho Gambo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Godbless Lema wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wamekutana katika mgahawa wa Safari Bistro jijini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Wawili hao ambao wamekuwa na mchuano mkali kuwani jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 wamekutana mgahawani hapo leo Jumanne 29 Septemba 2020.

Lema anatetea jimbo hilo ambalo ameliongoza kwa miaka kumi mfululizo huku Gambo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha akijitosa kwa mara ya kwanza kutaka kurejesha jimbo hilo chini ya himaya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Wanasiasa hao, wamepiga picha kadhaa wakiwa kwenye mgahawa huo na kila mmoja ameiweka kwenye kuraza zake za mitandao ya kijamii na kuiandikia maelezo ya kufarijiana kwa kile kitakachotokea baada ya uchaguzi mkuu.

“Leo tumekutana mbunge ninaeingia madarakani na mbunge aliyemaliza muda wake! Ameniambia kuwa hajawahi kuwa na uchaguzi mgumu kama mwaka huu na amejiandaa kisaikolojia.”

“CCM ni chama kubwa hatuwezi kukosa kazi ya kumpa. Hakika nyumbani kumenoga!,” ameandika Gambo

Wakati Gambo akiandika hivyo kwenye ukurasa wake wa Twitter, mshindani wake mkubwa Lema, ameweka picha Instagram na kuandika “nimekutana na huyu kijana hapa Safari Bistro cafe… akaomba picha, nikasema ni sawa tu, kwani akose Ubunge hata na picha na mimi wajameni…hali yake ni ya majonzi sana.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!