Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Papa Francis atoa wito
Habari Mchanganyiko

Papa Francis atoa wito

Papa Francis, Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki duniani
Spread the love

PAPA Francis, Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki duniani amesema, dunia haiwezi kupuuza ubaguzi wa rangi na kutengwa kwa watu. Inaripoti Mitandao ya kimataifa …(endelea)

Pia, ametoa wito wa kusimamisha uharibifu akisema, si sahihi na haivumiliki kutenda vurugu na uharibifu.

“Hatuwezi kujitia upofu kuhusu ubaguzi na kutengwa, lakini si sahihi kuendesha vurugu na uharibifu,” amesema Papa Francis leo tarehe 3 Juni 2020 akieleza hisia zake kuhusu kinachoendelea nchini Marekani.

Akitumia lugha ya Kiingereza amesema, analiombea Mungu taifa hilo lirejee katika hali ya amani na umoja.

Pia, amesisitiza umuhimu wa kuwa pamoja na kufikia muafaka kuhusu kile kilichotendeka ndani ya taifa hilo.

Taarifa za mchana huu leo Jumatano zinaeleza, maandamano nchini humo yanazidi kushika kasi huku vitendo vya uporaji na vurugu vikipungua kwa kiasi kikubwa.

Taarifa zinaeleza, miji ya Houston, Texas kumekuwa na maandamano makubwa zaidi kuwahi kutokea. Maeneo mengine yameanzisha maandamano kupinga mauaji ya Floyd.

Houston, eneo ambalo Floyd atazikwa, meya wa jiji hilo, Sylvester Turner amewaambia waandamanaji “Floyd hakufa bure,” kwamba ameacha somo Marekani.

Waandamaji katika Miji ya Los Angeles, Philadelphia, Atlanta na Seattle wameendelea kuvutana na vyombo vya usalama huku kukiwa hakuna dalili ya kupoa kwa maandamano hayo.

Matumizi makubwa ya gesi na maji kuwasha yameripotiwa kwenye miji ya Seattle, Portland na Atlanta

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Balile aukwaa uenyekiti wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

Habari Mchanganyiko

Jeshi la Uhifadhi kujengewa uwezo zaidi

Spread the love  WIZARA ya Maliasili na Utalii imejipanga vyema kuendelea kulijengea...

Habari Mchanganyiko

Wanavyuo Dodoma waonja utamu wa chimbo la nyuki

Spread the love  TAMASHA la Chimbo la Nyuki lililofanyika katika Ukumbi wa...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

error: Content is protected !!