Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko RC Mbeya sasa kuchapa viboko wasiofunga ndoa
Habari Mchanganyiko

RC Mbeya sasa kuchapa viboko wasiofunga ndoa

Albert Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya
Spread the love

ALBERT Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ametangaza kuwachapa bakora wanaume na wanawake wasiofunga ndoa. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Chalamila ametangaza kampeni hiyo kufuatia mijadala iliyoibuka mitandaoni hivi karibuni, juu ya changamoto ya wanawake wengi kutoolewa, ambapo baadhi ya wananchi wakinyooshea vidole wanaume kwamba wamekuwa wagumu kuoa.

Mkuu huyo wa wilaya ameeleza, mwanamke atakayekutwa hajaolewa, na mwanaume atakayekutwa hajaoa, atatatindwa bakora ili akatafute mume au mke.

“Maana siku hizi tunaanza kutumia viboko katika kila jambo, hata tukikuta umekaa pale nyumbani huolewi ni bakora tu, nenda katafute mume.

“Tunakuona umekee pale nyumbani huoi ni bakora tu nenda katatufute mke. Kuna umri ambao unatosha lazima uchangamshwe kwa hiyo viboko vinasaidia,” amesema Chalamila.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

error: Content is protected !!