Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko RC Mbeya sasa kuchapa viboko wasiofunga ndoa
Habari Mchanganyiko

RC Mbeya sasa kuchapa viboko wasiofunga ndoa

Albert Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya
Spread the love

ALBERT Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ametangaza kuwachapa bakora wanaume na wanawake wasiofunga ndoa. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Chalamila ametangaza kampeni hiyo kufuatia mijadala iliyoibuka mitandaoni hivi karibuni, juu ya changamoto ya wanawake wengi kutoolewa, ambapo baadhi ya wananchi wakinyooshea vidole wanaume kwamba wamekuwa wagumu kuoa.

Mkuu huyo wa wilaya ameeleza, mwanamke atakayekutwa hajaolewa, na mwanaume atakayekutwa hajaoa, atatatindwa bakora ili akatafute mume au mke.

“Maana siku hizi tunaanza kutumia viboko katika kila jambo, hata tukikuta umekaa pale nyumbani huolewi ni bakora tu, nenda katafute mume.

“Tunakuona umekee pale nyumbani huoi ni bakora tu nenda katatufute mke. Kuna umri ambao unatosha lazima uchangamshwe kwa hiyo viboko vinasaidia,” amesema Chalamila.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!