Jeshi la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limesema hivyo kwa kuwa, madereva wavamizi wa barabara hizo imeongezeka maradufu.
SACP Lazaro Mambosasa, kamanda wa polisi wa kanda huyo leo tatehe 1 Oktoba 2019 ametoa taarifa hiyo baada ya kujiridhisha kwenye oparesheni maalum ya kukamata magari iliyoanza tarehe 19 Septemba 2019.
Mambosasa amesema, kuna baadhi ya magari ya umma na binafsi yanatumia barabara maalumu za mabasi yaendayo kasi, wakidhani watalipa faini.
“Mabasi haya yametengewa njia kwa matumizi maalum, ninajua watu wana salio la kutosha. Anaandaa pesa halafu anakwenda kuingia kwenye mwendokasi akitegemea atalipa faini 30,000.
“Katika mwendokasi sitakubali kutoza faini, hatutatoza faini hatupo kwa ajili ya kutafuta fedha, tunachotaka ni kuweka nidhamu ya matumizi sahihi ya barabara hiyo,” amesema.
Aidha ametoa wito kwa madereva wote hasa kuhakikisha wanatii sheria na taratibu za barabara hiyo ili kuepukana na kadhia hiyo.
Katika oparesheni hiyo, jumla ya magari 50 yamekamatwa huku 19 yakiwa mali ya serikali huku 31 yakiwa ya watu binafsi.
Leave a comment