Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi watatu wafariki ajalini Rufiji
Habari Mchanganyiko

Polisi watatu wafariki ajalini Rufiji

Spread the love

ASKARI watatu wameripotiwa kufariki katika ajali ya gari ya Polisi mkoa wa kipolisi Rufiji iliyotokea baada ya gurudumu la nyuma la gari hiyo kupasuka na kusababisha gari kupinduka. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

SACP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini leo amewaambia waandishi wa habari kuwa ajali hiyo imetokea jana tarehe 25 Julai 2019 majira ya saa saba mchana katika kijiji cha Kilimahewa wilayani Mkuranga, Rufiji. 

Gari hilo Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili PT. 3822 lilikuwa likitokea Ikwiriri kuelekea Kijiji cha Mwalusembe, lilipasuka gurudumu moja la nyumba upande wa kulia na kusababisha kupinduka.

“Askari waliofariki kwenye ajali hiyo ni aliyekuwa Afisa Mnadhimu Rufiji, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Issah Bukuku na Inspekta Esteria wa Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Kipolisi Rufiji pamoja na namba G.1132 PC Lameck wa Kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) mkoani humo,” amesema.

Waliojeruhiwa ni F.7167 PC Ibrahim ambaye ndio alikuwa dereva wa gari hilo pamoja na F.7651 PC Mgusi wa ofisi ya Kamanda wa Polisi Rufiji.

SACP Misime amesema kuwa majeruhi wote wawili wamefikishwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

error: Content is protected !!