Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Mwakyembe atonesha vidonda vya Azory
Habari Mchanganyiko

Dk. Mwakyembe atonesha vidonda vya Azory

Spread the love

WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, amepuuza kilicho cha muda mrefu cha wadau wa habari nchini cha kutaka kuelezwa mahali aliko, mwandishi wa gazeti la Mwananchi, Azory Gwanda. Anaripoti Mwandishi Wetu kutoka Dodoma … (endelea).

Akizungumza bungeni leo Jumanne, Dk. Mwakyembe, ametaka kupuuzwa kwa watu wanaotaka ripoti kamili ya kupotea kwa Azory. Alikuwa ahitimisha mjadala wa bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha ujao wa fedha.

Mteule huyo wa Rais John Magufuli, amedai kushangazwa kwake na wanaofuatilia mahali aliko Gwanda, na kuongeza, “kama kupotea, waliopotea wako wengi.”

Azory Gwanda ametoweka katika mazingira ya kutatanisha tokea tarehe 21 Novemba 2017. Mpaka sasa, hakua ripoti yoyote iliyotolewa kutoka chombo chochote cha ulinzi na usalama juu ya kupotea kwake.

Mke wake, Anna Pinoni, alinukuliwa akisema, “…watu wapatao wanne, wakiwa kwenye gari aina ya Toyota Land Cruiser, yenye rangi nyeupe, walimchukua mume wake (Azory Gwanda), kutoka katikati ya mji huo, mahali ambapo hupendelea kukaa.

“Kwamba, aliporudi nyumbani alikuta vitu vimezagaa, ishara kuwa waliipekua nyumba yao.”

Mwandishi huyo mahiri wa habari, alikuwa akiishi na kufanyia shughuli zake katika mji mdogo wa Kibiti, mkoani Pwani.

Alikuwa mmoja wa waaandishi wa kwanza kabisa wa habari, kuripoti kwa kina, juu ya mfululizo wa mauwaji, yaliyokuwa yakitekelezwa katika eneo hilo.

Akitetea hoja yake ya kutaka wananchi kipuuza taarifa za kumtafuta mwandishi huyo, Dk. Mwakyembe amesema, kuna watu wengi wamepotea katika eneo hilo, wakiwemo vongozi wa serikali.

Ameapa kuwa “serikali itaendelea kuwadhibiti watu wanaokiuka utoaji wa maoni, kwa kuwa hakuna uhuru usiokuwa na mipaka.” Hakufafanua.

Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wa kisiasa, wanaitafsri kauli yake kuwa yawezekana kwa kuwa serikali ina mikono mirefu, inafahamu ya kupotea kwa mwandishi huyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

error: Content is protected !!