Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Lugola: Kamateni wanaomtukana rais
Habari Mchanganyiko

Lugola: Kamateni wanaomtukana rais

Kangi Lugola Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Spread the love

KANGI Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ameliagiza Jeshi la Polisi, wakuu wa mikoa pamoja na wakuu wa wilaya kuwasweka ndani wanasiasa wataofanya mikutano ya ndani na kumtukana rais. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Lugola ametoa agizo holo wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Kilosa Town, Morogoro.

Amewataka viongozi hao kushirikiana na polisi kukamata wanasiasa wanaofanya mikutano ya ndani na kuvunja sheria za nchi.

Lugola ameelekeza kuwa, wanasiasa hao wachunguzwe wanapofanya mikutano ya ndani kwa kuwa baadhi yao hutumia mikutano hiyo kumtukana Rais John Magufuli pamoja na kutoa kauli zinazochonganisha wananchi na serikali yao.

Amesema, hatomvumilia kiongozi yoyote wa chama cha siasa atakayefanya mikutano ya hadhara au kutumia mikutano ya ndani kukiuka sheria za nchi.

Amewataka wanasiasa kutii agizo la seriali la kutofanya mikutano ya hadhara hadi pale kampeni zitakapoanza katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Balile aukwaa uenyekiti wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

Habari Mchanganyiko

Jeshi la Uhifadhi kujengewa uwezo zaidi

Spread the love  WIZARA ya Maliasili na Utalii imejipanga vyema kuendelea kulijengea...

Habari Mchanganyiko

Wanavyuo Dodoma waonja utamu wa chimbo la nyuki

Spread the love  TAMASHA la Chimbo la Nyuki lililofanyika katika Ukumbi wa...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

error: Content is protected !!