Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Lugola: Kamateni wanaomtukana rais
Habari Mchanganyiko

Lugola: Kamateni wanaomtukana rais

Kangi Lugola Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Spread the love

KANGI Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ameliagiza Jeshi la Polisi, wakuu wa mikoa pamoja na wakuu wa wilaya kuwasweka ndani wanasiasa wataofanya mikutano ya ndani na kumtukana rais. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Lugola ametoa agizo holo wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Kilosa Town, Morogoro.

Amewataka viongozi hao kushirikiana na polisi kukamata wanasiasa wanaofanya mikutano ya ndani na kuvunja sheria za nchi.

Lugola ameelekeza kuwa, wanasiasa hao wachunguzwe wanapofanya mikutano ya ndani kwa kuwa baadhi yao hutumia mikutano hiyo kumtukana Rais John Magufuli pamoja na kutoa kauli zinazochonganisha wananchi na serikali yao.

Amesema, hatomvumilia kiongozi yoyote wa chama cha siasa atakayefanya mikutano ya hadhara au kutumia mikutano ya ndani kukiuka sheria za nchi.

Amewataka wanasiasa kutii agizo la seriali la kutofanya mikutano ya hadhara hadi pale kampeni zitakapoanza katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!