Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Lugola: Kamateni wanaomtukana rais
Habari Mchanganyiko

Lugola: Kamateni wanaomtukana rais

Kangi Lugola Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Spread the love

KANGI Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ameliagiza Jeshi la Polisi, wakuu wa mikoa pamoja na wakuu wa wilaya kuwasweka ndani wanasiasa wataofanya mikutano ya ndani na kumtukana rais. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Lugola ametoa agizo holo wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Kilosa Town, Morogoro.

Amewataka viongozi hao kushirikiana na polisi kukamata wanasiasa wanaofanya mikutano ya ndani na kuvunja sheria za nchi.

Lugola ameelekeza kuwa, wanasiasa hao wachunguzwe wanapofanya mikutano ya ndani kwa kuwa baadhi yao hutumia mikutano hiyo kumtukana Rais John Magufuli pamoja na kutoa kauli zinazochonganisha wananchi na serikali yao.

Amesema, hatomvumilia kiongozi yoyote wa chama cha siasa atakayefanya mikutano ya hadhara au kutumia mikutano ya ndani kukiuka sheria za nchi.

Amewataka wanasiasa kutii agizo la seriali la kutofanya mikutano ya hadhara hadi pale kampeni zitakapoanza katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!