Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mo aitwa Singida, wazee wataka kufanya yao
Habari MchanganyikoTangulizi

Mo aitwa Singida, wazee wataka kufanya yao

Spread the love

MFANYABIASHARA maarufu Mohammed Dewji ‘Mo’ ameombwa kwenda mkoani Singida ili apozwe machungu. Anaandika Mwandishi Maalum … (endelea).

Akizungumza na wanahabari kwenye viwanja vya CCM Singida baada ya kupatikana Mo, Mzee Juma Mwandoghwe amesema, wazee wanataka kumchinjia mbuzi na kufanya dua kutokana na kutendewa unyama wa kutekwa na watu wasiojulikana.

Mo ni mzaliwa wa Singida ambaye ameongoza jimbo hilo kwa miaka 10 (2005-2015).

Hata hivyo, haijafahamika kama Mo ataitikia wito huo.

Akiwakilisha wazee wenzake, Mzee Mwandoghwe amesema kuwa, Mo anapaswa kutulizwa na kupewa faraja.

Mzee Mwandoghwe amesema kuwa, Mo yupo Dar es Salaam kibiashara na Singida ndio nyumbani hivyo wanao wajibu kwa kijana wao aliyewahi kuwaongoza kwenye jimbo hilo la Singida Mjini.

Mzee Mwandoghwe ameeleza kulaani ukatili alikfanyiwa Mo na kueleza kuwa kitendo hicho ni cha kinyama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

error: Content is protected !!