Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko DART yatoa tamko kuhusu hujuma za madereva wa Udart
Habari MchanganyikoTangulizi

DART yatoa tamko kuhusu hujuma za madereva wa Udart

Mabasi yaendayo kasi
Spread the love

WAKALA wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) umesema madereva wa kampuni ya mtoa huduma, (Udart) waliohusika kufanya hujuma ya kuzuia mabasi yaliyokuwa yameegeshwa katika karakana ya Jangwani, na kusababisha adha ya usafiri siku ya Jumatano ya Oktoba 10 2018, wamechukuliwa hatua. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kupitia tamko lake iliotoa leo tarehe 12 Oktoba 2018, DART imesema madereva hao wamechukuliwa hatua za kisheria na vyombo vya usalama, huku ikitoa onyo kwa wafanyakazi wa mfumo wa DART watakaojihusisha na hujuma watachukuliwa hatua ikiwemo kuachishwa kazi.

“Serikali imetoa onyo kali kwa wafanyakazi katika mfumo wa DART watakaojihusisha na hujuma na kuwa hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa ikiwemo kuachishwa kazi,” inaeleza sehemu ya tamko hilo.

Katika hatua nyingine, DART imeomba radhi watumiaji wa mabasi yanayotoa huduma katika mfumo wa DART kwa usumbufu wlaiopata, huku ikiahidi kuhakikisha kuboresha huduma zake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

error: Content is protected !!