Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko DART yatoa tamko kuhusu hujuma za madereva wa Udart
Habari MchanganyikoTangulizi

DART yatoa tamko kuhusu hujuma za madereva wa Udart

Mabasi yaendayo kasi
Spread the love

WAKALA wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) umesema madereva wa kampuni ya mtoa huduma, (Udart) waliohusika kufanya hujuma ya kuzuia mabasi yaliyokuwa yameegeshwa katika karakana ya Jangwani, na kusababisha adha ya usafiri siku ya Jumatano ya Oktoba 10 2018, wamechukuliwa hatua. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kupitia tamko lake iliotoa leo tarehe 12 Oktoba 2018, DART imesema madereva hao wamechukuliwa hatua za kisheria na vyombo vya usalama, huku ikitoa onyo kwa wafanyakazi wa mfumo wa DART watakaojihusisha na hujuma watachukuliwa hatua ikiwemo kuachishwa kazi.

“Serikali imetoa onyo kali kwa wafanyakazi katika mfumo wa DART watakaojihusisha na hujuma na kuwa hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa ikiwemo kuachishwa kazi,” inaeleza sehemu ya tamko hilo.

Katika hatua nyingine, DART imeomba radhi watumiaji wa mabasi yanayotoa huduma katika mfumo wa DART kwa usumbufu wlaiopata, huku ikiahidi kuhakikisha kuboresha huduma zake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!