Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanesco, REA wapigwa marufuku kuagiza vifaa nje
Habari MchanganyikoTangulizi

Tanesco, REA wapigwa marufuku kuagiza vifaa nje

Makao Mkuu wa Tanesco, Ubungo Dar es Salaam kabla hayajavunjwa
Spread the love

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) limetakiwa kusitisha uagizaji wa viunganishi vya miundombinu ya umeme (Accessories) kutoka nje ya nchi ifikapo mwezi Novemba mwaka huu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea)

Agizo hilo lilitolewa jana tarehe 6 Agosti, 2018 na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani wakati alipotembelea Kiwanda cha uzalishaji viunganishi cha Auto Mech Ltd kilichopo Tabata jijini Dar es Salaam.

Dkt. Kalemani alitoa agizo hilo baada ya kujiridhisha kwamba kiwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha viunganishi vya kutosha, ambapo aliitaka Tanesco kununua viunganishi vinavyotengenezwa hapa nchini.

 “Nimekuja hapa ili kujiridhisha kama Kiwanda hiki kina uwezo wa kuzalisha viunganishi vya kutosha, nimejiridhisha kuwa, kiwanda hiki kina uwezo wa kuzalisha viunganishi hivyo, kwa hiyo nimetoa miezi mitatu ili TANESCO, REA na Wakandarasi wote kwa pamoja wajiandae sasa kunua vifaa hivi nchini.” Alisema Waziri Kalemani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

error: Content is protected !!