Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanesco, REA wapigwa marufuku kuagiza vifaa nje
Habari MchanganyikoTangulizi

Tanesco, REA wapigwa marufuku kuagiza vifaa nje

Makao Mkuu wa Tanesco, Ubungo Dar es Salaam kabla hayajavunjwa
Spread the love

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) limetakiwa kusitisha uagizaji wa viunganishi vya miundombinu ya umeme (Accessories) kutoka nje ya nchi ifikapo mwezi Novemba mwaka huu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea)

Agizo hilo lilitolewa jana tarehe 6 Agosti, 2018 na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani wakati alipotembelea Kiwanda cha uzalishaji viunganishi cha Auto Mech Ltd kilichopo Tabata jijini Dar es Salaam.

Dkt. Kalemani alitoa agizo hilo baada ya kujiridhisha kwamba kiwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha viunganishi vya kutosha, ambapo aliitaka Tanesco kununua viunganishi vinavyotengenezwa hapa nchini.

 “Nimekuja hapa ili kujiridhisha kama Kiwanda hiki kina uwezo wa kuzalisha viunganishi vya kutosha, nimejiridhisha kuwa, kiwanda hiki kina uwezo wa kuzalisha viunganishi hivyo, kwa hiyo nimetoa miezi mitatu ili TANESCO, REA na Wakandarasi wote kwa pamoja wajiandae sasa kunua vifaa hivi nchini.” Alisema Waziri Kalemani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

error: Content is protected !!