SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) limetakiwa kusitisha uagizaji wa viunganishi vya miundombinu ya umeme (Accessories) kutoka nje ya nchi ifikapo mwezi Novemba mwaka huu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea)
Agizo hilo lilitolewa jana tarehe 6 Agosti, 2018 na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani wakati alipotembelea Kiwanda cha uzalishaji viunganishi cha Auto Mech Ltd kilichopo Tabata jijini Dar es Salaam.
Dkt. Kalemani alitoa agizo hilo baada ya kujiridhisha kwamba kiwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha viunganishi vya kutosha, ambapo aliitaka Tanesco kununua viunganishi vinavyotengenezwa hapa nchini.
“Nimekuja hapa ili kujiridhisha kama Kiwanda hiki kina uwezo wa kuzalisha viunganishi vya kutosha, nimejiridhisha kuwa, kiwanda hiki kina uwezo wa kuzalisha viunganishi hivyo, kwa hiyo nimetoa miezi mitatu ili TANESCO, REA na Wakandarasi wote kwa pamoja wajiandae sasa kunua vifaa hivi nchini.” Alisema Waziri Kalemani.
Leave a comment