Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mambosasa awatoa hofu wanyoa ‘viduku’
Habari Mchanganyiko

Mambosasa awatoa hofu wanyoa ‘viduku’

Spread the love

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amekanusha taarifa kuhusu kukamata wanyoa viduku, wavaa vimini zinazoendelea kusambaa. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Kamanda Mambosasa ameyasema hayo leo ofisini kwake akizungumza na waandishi wa habari huku kukiwa na habari zilizochapishwa katika Gazeti la Nipashe lenye kichwa cha habari ‘Polisi yakamata wavaa vimini, kunyoa viduku’.

“Mwandishi huyu jana alikuwa ananiambia nina operation gani dhidi ya wanaovaa nguo fupi na nilimjibu wazi, nilieleza swala la nguo fupi inategemea wapi umevalia, sikuishia wapi nikasema nitashangaa kuona mtu anavaa nguo fupi katika maeneo ya staha.

Amesema, alichokisema ni kwamba kuna matendo mtu anaweza akayafanya ambayo ni kinyume cha maadili ya Mtanzania, ambapo hata yeye kama kamanda wa mkoa analiona lina machukizo lakini si rahisi kuwakamata watu wanaovaa hivyo, lakini wanaofanya ufuska kwa kujipatia mapato hilo ni kosa la jinai.

“Huu ni uzushi mwandishi amechukua maneno akaweka kinywani kwangu ili niyaseme akauze gazeti, amejikosesha heshima, kukaa koridoni, kukaa kichakani harafu ukatengeza story harafu ukaenda kuiuzia Gazeti ni kujikosesha heshima,…..yaliyoandikwa hayakusemwa na Jeshi la Polisi na ninamtaka arudi kwa watanzania aombe radhi ili kuondoa usumbufu unaojitokeza.

“Sikueleza kwamba kuna msako unaoendelea wa kukamata watu waliovaa nguo fupi ispokuwa nilichokisema kuna matendo mtu anaweza kuyafanya ambayo ni kinyume cha maadili ya Tanzania”.

Hivi karibuni gazeti hilo liliomba radhi kwa kuandika taarifa zilizoelezwa kuwa ni za uzushi kuhusu rais Magufuli na lilijifungia lenyewe kuchapa gazeti lake la ‘Nipashe Jumapili’ kwa muda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!