Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mambosasa awatoa hofu wanyoa ‘viduku’
Habari Mchanganyiko

Mambosasa awatoa hofu wanyoa ‘viduku’

Spread the love

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amekanusha taarifa kuhusu kukamata wanyoa viduku, wavaa vimini zinazoendelea kusambaa. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Kamanda Mambosasa ameyasema hayo leo ofisini kwake akizungumza na waandishi wa habari huku kukiwa na habari zilizochapishwa katika Gazeti la Nipashe lenye kichwa cha habari ‘Polisi yakamata wavaa vimini, kunyoa viduku’.

“Mwandishi huyu jana alikuwa ananiambia nina operation gani dhidi ya wanaovaa nguo fupi na nilimjibu wazi, nilieleza swala la nguo fupi inategemea wapi umevalia, sikuishia wapi nikasema nitashangaa kuona mtu anavaa nguo fupi katika maeneo ya staha.

Amesema, alichokisema ni kwamba kuna matendo mtu anaweza akayafanya ambayo ni kinyume cha maadili ya Mtanzania, ambapo hata yeye kama kamanda wa mkoa analiona lina machukizo lakini si rahisi kuwakamata watu wanaovaa hivyo, lakini wanaofanya ufuska kwa kujipatia mapato hilo ni kosa la jinai.

“Huu ni uzushi mwandishi amechukua maneno akaweka kinywani kwangu ili niyaseme akauze gazeti, amejikosesha heshima, kukaa koridoni, kukaa kichakani harafu ukatengeza story harafu ukaenda kuiuzia Gazeti ni kujikosesha heshima,…..yaliyoandikwa hayakusemwa na Jeshi la Polisi na ninamtaka arudi kwa watanzania aombe radhi ili kuondoa usumbufu unaojitokeza.

“Sikueleza kwamba kuna msako unaoendelea wa kukamata watu waliovaa nguo fupi ispokuwa nilichokisema kuna matendo mtu anaweza kuyafanya ambayo ni kinyume cha maadili ya Tanzania”.

Hivi karibuni gazeti hilo liliomba radhi kwa kuandika taarifa zilizoelezwa kuwa ni za uzushi kuhusu rais Magufuli na lilijifungia lenyewe kuchapa gazeti lake la ‘Nipashe Jumapili’ kwa muda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!