Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Ummy: Serikali isiwe kikwazo
Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy: Serikali isiwe kikwazo

Waziri wa Nchi Ofisi a Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Ummy Mwalimu
Spread the love

TAASISI za serikali zinazohusika na masuala ya ukaguzi na udhibiti wa bidhaa, zimetakiwa kutokuwa kikwazo kwa maendeleo ya wajasiriamali na ujenzi wa viwanda hapa nchini. Anaripoti Regina Kelvin…(endelea).

Agizo hilo limetolewa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akihutubia kwenye mkutano wa wadau wa kujadili mchango wa taasisi za serikali katika kuanzisha na kuboresha viwanda vya chakula nchini.

Waziri Ummy amesema Shirika la Viwango nchini (TBS), Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA) na ofisi ya mkemia mkuu wa serikali kusikilizana katika utekelezaji wa majukumu yao ili kuondoa vikwazo kwa wajasiriamali na ujenzi wa viwanda.

“TBS, TFDA na mamlaka nyingine inabidi msikilizane ili kuondoa vikwazo kwa wafanyabiashara na wawekezaji,” amesema.

Naye Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema serikali itanedelea kuondoa changamoto za wajasiriamali na wawekezaji wa viwanda, lakini amewataka wajasiriamali hao kutobweteka katika uzalishajiwa bidhaa zenye ubora.

“Tunajenga vianda kwa ajili ya kutoa ajira, kuanzisha bishaa zenye ubora na viwango vya kukidhi matakwa ya watanzania na soko la nje ya nchi. Tunachopaswa kufanya tutengeneze viwango vya kiuhalisia. Tunawasaidia lakini Msibweteke,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!