Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Ummy: Corona ipo
Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy: Corona ipo

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya
Spread the love

LICHA ya ripoti ya maambukizi ya virisi vinavyosababisha ugonjwa wa corona kupungua nchini, ugonjwa huo haujaisha nchini. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya leo tarehe 1 Juni 2020, jijini Tanga wakati wa ufunguzi wa jengo la ofisi za Makao Makuu ya Bodi ya Mkonge Tanzania.

 “Tunamshukuru Mungu hali ni nzuri, Tanga hatuna mgonjwa wa corona, kituo kilichokuwa kinatumika kwa wagonjwa wa corona kimefungwa.

“Amana tuna wagonjwa  watatu, Mloganzila  mmoja, Mwanza hakuna mgonjwa. Tunamshukuru Mungu, hata hivyo corona ipo, tuendelee kuchukua tahadhari kujikinga,” amesema Waziri Ummy.

Amesema, Tanzania imefanikiwa katika kudhibiti kasi ya maambukizi ya ugonjwa huo “corona tumeishinda Tanzania, ukiangalia wenzetu, unajiuliza hivi Tanzania tuna nini? asante Mwenyezi Mungu kwa kutuokoa,” amesema Waziri Ummy.

Mara ya kwanza Tanzania iliripoti kisa chake cha kwanza cha ugonjwa wa Covid-19, tarehe 16 Machi 2020, ambapo siku moja baadae ilitangaza kufunga baadhi ya shughuli zenye mikusanyiko ya watu wengi, ili kudhibiti maambukizi ya ugonjwa huo.

Miongoni mwa shughuli zilizofungwa  tarehe 17 na 18 Machi 2020 ni, michezo, shule na vyuo vya kati na vikuu, pamoja na shughuli za kijamii.

Lakini Mei mwaka huu, Rais John Magufuli alitangaza kufunguliwa kwa vyuo pamoja na shughuli za michezo.

Wakati akitangaza kufunguliwa kwa shughuli hizo, Rais Magufuli alisema hatua hiyo imechukuliwa baada ya maambukizi ya Covid-19, kupungua kwa kasi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!