Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waliokula Bil 1.5 kukiona cha moto
Habari za Siasa

Waliokula Bil 1.5 kukiona cha moto

Spread the love

RAIS John Magufuli ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha vinawachukulia hatua kali watu wote waliohusika katika kufanya ubadhilifu wa zaidi ya Sh. 1.5 bilioni ya mradi wa maji wa Ntomoko. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Agizo hilo alilitoa wakati wa ufunguzi wa barabara ya Dodoma Manyara yenye urefu wa kilometa 251 iliyozinduliwa katika eneo la Bicha wilayani Kondoa mkoani hapa ambayo itaongeza fursa mbalimbali za kiuchumi kwa wananchi wa mikoa hiyo miwili.

Akiwahutubia wananchi wa Kondoa na Manyara, muda mfupi baada ya kupatiwa taarifa ya mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhandisi Bilinithi Mahenge, kuelezea kuwa kuna ubadhirifu wa zaidi ya Sh. bilioni moja na nusu zilizopotea katika mradi wa maji wa Ntomoko na kuwakosesha huduma ya maji wananchi wa wilaya ya Kondoa na Chemba.

Mradi huo wa kutandika mabomba ya kusambazia maji kuwafikia wananchi ambapo waliopewa dhamana hiyo badala ya kutandika mabomba ambayo yanauwezo mkubwa wa kufikisha maji wao wakaweka mabomba madogo ambayo hayana uwezo.

“Kama ni kuchomoka basi wachomoke wale wote waliofanya ubadhirifu wa mradi huu kwani wanawapa shida wananchi wanyonge ambao walikuwa wapate huduma ya maji tokea mwaka 1980,” alisisitiza Rais Magufuli.

Aidha kwa upande mwingine Rais Magufuli akawataka viongozi wa wilaya hiyo kuacha migogoro ya wao kwa wao na kuwa migogoro inachangia kushindwa kuwapelekea wananchi huduma za maendeleo kwa wakati na yeye hakuwatuma kwenda kuibua migogoro hiyo.

Kwa upande wake Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, Akinwim Adesina aliahidi neema kwa jiji jipya la Dodoma na serikali kwa ujumla kwamba atatoa ushirikiano kuhakikisha serikali na jiji hilo wanapata fedha za miradi.

Amesema kuwa barabara hiyo itafungua milango ya kiuchumi kwa lango la Kaskazini mwa Afrika na Kusini ambapo hiyo itakuwa fursa pana kwa wananchi wa mataifa nane barani humo ambayo barabara hiyo inapita kutoka Cape Town hadi Cairo nchini Misri.

Nae Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa amesema kuwa barabara hiyo yenye urefu wa km. 251 imejengwa kwa jumla ya Sh. 378.4 bilioni kati ya hizo fedha za ndani Sh. 107.6 bilioni na zilizobakia zimechangiwa na wafadhili Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB) na Shirika la Maendeleo la Japani (JICA).

Pauline Gekul amchokonoa JPM

Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekuli amemtaka Rais John Magufuli kuingilia kati mgogoro uliopo kati ya wananchi na Chama cha Mapinduzi (CCM) kuhusiana na stendi ya mabasi.

Amesema pamoja na kujengwa barabara ambayo inaunganisha Dodoma na Babati ambayo itafungua fursa kubwa kwa wananchi lakini bado kuna changamoto ya stendi ambayo imekuwa ikileta utata kati ya wananchi wa CCM kwa kudai kuwa eneo hilo ni la kwao.

“Mheshimiwa Rais kwanza kabisa nishukuru kwa maendeleo ya barabara hii ambayo unaizindua leo ambayo wananchi wa Babati watajiongezea kipato kwa kutumia barabara hiyo.

“Na kama unavyosema kuwa maendeleo hayana vyama hivyo naomba uingilie kati na kutatua mgogoro wa stendi kwa sasa najua magari yatakuwa mengi lakini hakuna stendi kwani hiyo kwa sasa imeonekana kuwa ni ya chama cha mapinduzi badala ya halmashauri.

“Sasa naomba utuachie stendi hiyo ili wananchi waendelee kuitumia na kuongeza kipato kwa halmashauri hiyo na badala yake wanachama wa CCM watapatiwa kiwanja kingine ili waweze kujenga wanachokitaka,” amesema Gekul.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!