Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mdogo wa Heche adaiwa kuuwawa mikononi mwa Polisi
Habari za SiasaTangulizi

Mdogo wa Heche adaiwa kuuwawa mikononi mwa Polisi

Wananchi wa Sirari wakiwa nje ya kituo cha Polisi kinachodaiwa kumuua kijana Suguta
Spread the love

MDOGO wa Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche aitwaye Chacha Heche Suguta, adaiwa kuuwawa akiwa chini ya Jeshi la Polisi baada ya kukutwa akiwa jeraha la kuchomwa kisu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ndugu wa marehemu wanasema wakati alipokamatwa na Polisi alikuwa mzima kabisa. Muda huu mabomu ya machozi na risasi vinafurumushwa kuwafukuza wananchi kutoka kituoni.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, RPC Mwibambe amekiri askari wake kuhusika na mauaji hayo ya kijana huyo aliyezaliwa mwaka 1989. Chacha Suguta ni mdogo (upande wa Baba mdogo) wa Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche (Chadema).

John Heche anasema kuwa kijana huyo alikamatwa na Askari wa Jeshi la Polisi usiku wa jana akiwa Baa akiwa mzima kabisa.

Heche amesisitiza kuwa baada ya kufariki, Askari wa Polisi walitaka kuutupa mwili wake lakini ilishindikana kwa sababu eneo walilotegemea kuutupa kulikuwa na Mlinzi aliyewafukuza, ndipo walipoamua kuupeleka mwili wake kwenye chumba cha kuhifadhia maiti (Mortuary) ya Tarime.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!