Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mdogo wa Heche adaiwa kuuwawa mikononi mwa Polisi
Habari za SiasaTangulizi

Mdogo wa Heche adaiwa kuuwawa mikononi mwa Polisi

Wananchi wa Sirari wakiwa nje ya kituo cha Polisi kinachodaiwa kumuua kijana Suguta
Spread the love

MDOGO wa Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche aitwaye Chacha Heche Suguta, adaiwa kuuwawa akiwa chini ya Jeshi la Polisi baada ya kukutwa akiwa jeraha la kuchomwa kisu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ndugu wa marehemu wanasema wakati alipokamatwa na Polisi alikuwa mzima kabisa. Muda huu mabomu ya machozi na risasi vinafurumushwa kuwafukuza wananchi kutoka kituoni.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, RPC Mwibambe amekiri askari wake kuhusika na mauaji hayo ya kijana huyo aliyezaliwa mwaka 1989. Chacha Suguta ni mdogo (upande wa Baba mdogo) wa Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche (Chadema).

John Heche anasema kuwa kijana huyo alikamatwa na Askari wa Jeshi la Polisi usiku wa jana akiwa Baa akiwa mzima kabisa.

Heche amesisitiza kuwa baada ya kufariki, Askari wa Polisi walitaka kuutupa mwili wake lakini ilishindikana kwa sababu eneo walilotegemea kuutupa kulikuwa na Mlinzi aliyewafukuza, ndipo walipoamua kuupeleka mwili wake kwenye chumba cha kuhifadhia maiti (Mortuary) ya Tarime.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!