WAGOMBEA kumi wa urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 wamechukua fomu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Fomu hizo zimeanza kutolewa tarehe 5 Agosti, 2020 Ofisi za NEC zilizopo nje kidogo ya Jiji la Dodoma eneo la Njedengwa na Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji mstaafu Semistocles Kaijage.
Shughuli ya uchukuaji na urejeshaji wa fomu hizo, utahitimishwa tarehe 25 Agosti 2020, siku ambayo NEC itawateua waliokidhi vigezo vya kuteuliwa.
Hadi kufikia leo Jumamosi tarehe 8 Agosti, 2020, wagombea kumi wamekwisha kuchukua fomu hizo kati yao wanawake ni wawili.
Vyama vilivyochukua fomu hizo ni; Seif Maalim Seif (AAFP) na mgombea mwenza, Rashid Ligania Rai, Leopard Mahona wa NRA, Philip John Fumbo wa DP, Rais John Pombe Magufuli wa CCM na mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassan na Tundu Lissu wa Chadema na mgombea mwenza, Salum Mwalimu
Wengine ni; Mutamwega Bati Mgaiwa wa SAU, Qeen Cuthbert Sendiga wa ADC, Twalib Ibrahim Kadege kupitia UPDP, Cecilia Augustino Mwanga wa Demokrasia Makini, Bernard Membe wa ACT- Wazalendo na mgombea mwenza wake, Profesa Omar Fakih Hamad.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali.
Leave a comment