Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wafanyabiashara watakiwa kufuata sheria za miji
Habari Mchanganyiko

Wafanyabiashara watakiwa kufuata sheria za miji

Spread the love

SHIRIKA la kuwahudumia wakimbizi la Tanganyika (TCRS) lililopo mkoani hapa limewataka wafanyabiashara kutii sheria za miji na majiji zilizopo bila shuruti huku akiwaasa kufanya biashara kwa kujiwekea malengo na kuwa na nidhamu ya fedha. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Hayo yalisemwa jana na Msimamizi wa miradi wa Shirika la TCRS mkoa wa Morogoro, Rehema Samweli wakati  akizungumza katika mkutano wa wafanyabiashara wadogo ulioandaliwa  shirika hilo ukilenga kujadili hali halisi ya masoko kwa wafanyabiashara wadogo.

Rehema alisema, ni vema wakaacha tabia ya kufanya biashara kwa mazoea na kwa msemo wa bora siku ipite, bali wafanyeni biashara huku wakiwa wamejiwekea malengo madhubuti kwa ajili ya leo na kesho yao.

Alisema changamoto za wafanyabiashara ni nyingi na zinajulikana lakini aliwataka kwanza kutambua umuhimu wa kutii sheria ambazo zinawekwa na mamlaka lakini pia wawe na uvumilivu huku wote wakiwa na sauti moja yenye umoja.

Hata hivyo Rehema aliongeza kusema kuwa TCRS inatarajia kuanza kusaidia vikundi mbalimbali vya wafanyabiashara wadogo  wa mjini hapa kwa kuwaongezea mitaji ya biashara wanazozifanya katika vikundi vyao.

Alisema kuwasaidia kimikopo kutawafanya wafanyabiashara hao kuinuka na kuepokana na mlolongo mrefu wa masharti ya kupata mikopo na kutokopesheka kwa urais kutokana na kutokua na mali kubwa za ukopesheka kwenye vyombo vya kifedha kama dhamana.

Mmoja wa wafanyabiashara wadogo wa Manispaa ya Morogoro, Hassan Zuberi, alisema kuwa serikali na mashirika binafsi inapaswa kuwatazama wafanyabiashara wadogo kwa jicho la kuwainua kimaendeleo kwani ni kundi muhimu mno kwa maendeleo ya nchi.

Hata hivyo Zuberi alisema ni muhimu serikali ikaweka mikakati mizuri na kutoa mikopo kwa wingi na ikapunguza vigezo na masharti ya kupata mikopo ili vijana waweze kufanya biashara kwa tija huku wakikuza pato lao na Taifa kwa ujumla.

Akizungumzia suala la ajira kwa vijana wanaotoa vyuoni Zuberi alisema Kila siku vijana wanamaliza vyuo vikuu na ngazi nyingine za elimu lakini suala la ajira za kuajiriwa wengi wao wanakosa na hujikita katika kufanya biashara ndogo ndogo ambapo alisema Serikali bado inahitaia kufanya kitu ili kuimarisha suala la ajira kwa vijana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!