Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Utapataje mtoto bila… mkeo? – Rais Magufuli
Habari Mchanganyiko

Utapataje mtoto bila… mkeo? – Rais Magufuli

Spread the love

RAIS John Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) amehoji, mtu anawezaje kupata mtoto bila kusogeleana? Anaripoti Hamisi Mguta, Dodoma … (endelea).

Akizungumza baada ya kurejesha fomu ya kugomba kuteuliwa na chama chake –CCM – leo tarehe 30 Juni 2020, kwenye makao makuu ya chama hicho jijini Dodoma amesema, watu wameendelea kusogeleana na maisha yanakwenda.

Alikuwa akizungumzia utaratibu ambapo sasa unasisitizwa duniani wa kukaa umbali wa zaidi ya mita moja, ili kuepuka kueneza virusi vinavyosababisha homa ya mapafu vya corona (COVID-19).

“Unaambiwa usimsogelee mtu mpaka mita moja, mke wako utaacha kumsogelea? au mume wako, utapataje mtoto bila kusogeleana? Nasema uongo?” Rais Magufuli alihoji ambapo alijibiwa “kweliiii!”

Amesema, Mungu ameendelea kusimamia taifa hili na hivyo kusaidia kupungua kwa maambukizi huku akisisitiza Watanzania kuendelea kumuomba Mungu.

“… na ndio maana sisi tukasema, tunaendelea kusogeleana kwa sababu Mungu wetu anatupenda na siku zote anasimama mbele…, leo tupo hapa hatujavaa chochote,” amesema.

Rais John Magufuli, Mwenyekiti wa CCM

Rais Magufuli amerejesha fomu hizo leo ambapo amepokelewa na kupokelewa na Dk. Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa chama hicho. Hafla hiyo fupi imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa CCM, serikali na wanachama wa chama hicho.

Zaidi ya wanachama milioni moja (1,000,000) wa CCM kutoka mikoa 30, wamejitokeza kumdhamini Rais Magufuli katika safari yake ya kusaka awamu ya pili ya kuliongoza taifa.

Rais Magufuli aliyechukua fomu ya kugombea urais wa Tanzania tarehe 17 Juni 2020, anarudisha fomu hiyo leo katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM jijini Dodoma.

Mkoa wa Tanga wamejitokeza wanachama 62,869, Tabora (29,486), Songwe (11,744), Simiyu (3,693), singida (13,452), Dodoma (44,415), Pwani (20,603), Rukwa (5,600), Ruvuma (56,350), Shinyanga (12,000), Arusha (22,706), Dar es Salaam (71,491).

Mtwara (7,569), Mwanza (17,810), Geita (89,595) na Iringa (12,542), Kagera (27,245), Katavi (5071), Morogoro (117,450), Kaskazini Pemba (2,575), Kaskazini Unguja (1,141), Kigoma (30,220), Kilimanjaro (23,434).

Mkoa wa Mjini (2,394), Kusini Pemba (350), Lindi (9,515), Mkoa wa Magharibi (1,005), Manyara (19,972), Mara (87,550) na Mbeya 19,972.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!