Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba, Yanga, Azam Matatani
Michezo

Simba, Yanga, Azam Matatani

Ofisi za TFF
Spread the love

SHIRIKISHO la mpira wa miguu Tanzania ‘TFF’, limepiga marufuku michezo yote ya kirafiki kwa klabu zote nchini mpaka pale itakapotoa kibali maalumu kutokana na timu hizo kutofuata masharti ya Wizara na Serikali juu ya ugonjwa wa Covid 19. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… endelea

Hivi karibuni serikali kupitia Wizara ya Michezo sambamba na Wizara ya Afya ilitoa muongozo maalumu kwa klabu na wamiliki wa viwanja katika kuchukua tahadhali dhidi ya ugonjwa wa Covid 19 baada ya kurejea kwa michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Katika taarifa iliyotoka ndani ya Shirikisho hili imeeleza kuwa TFF itakutana na klabu za Simba, Yanga, KMC na Transit Camp ambao walicheza michezo ya kirafiki hivi karibuni ambao ilionekan kuwa na dosari kubwa katika kuchukua hatua kukabiliana na maradhi ya Covid 19.

Klabu hizo zilicheza michezo hiyo ya kirafiki ili kujiweka sawa kuelekea michezo ya Ligi Kuu inayotarajia kuendelea juni 13, 2020 sambamba na Ligi daraja la kwanza.

Hivi karibuni klabu ya Azam Fc ilicheza mchezo wake wa kirafiki dhidi ya Transit Camp na kumalizika kwa sare, huku klabu ya Yanga ilipoteza mchezo dhidi ya KMC kwa mabao 3-0, huku Simba ilicheza michezo miwili ya kirafiki ndani ya siku moja.

Mchezo wa kwanza uliopigwa asubuhi kwenye uwanja MO Simba complex Arena dhidi ya Transit Camp na kuibuka na ushindi wa mabao 4-2 na katika mchezo mwengine uliofanyika jioni Simba iliwakaribisha KMC na kuibuka na ushindi wa mabao 3-1.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!