BODI ya Ligi imehailisha mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kati ya Yanga dhidi ya Simba uliokuwa uchezwe 18 Oktaba, 2020 na sasa utapigwa 7 Novemba, 2020 kutokana kuwepo kwa vikwazo vya usafiri vilivyowekwa na baadhi ya nchi mara baada ya kukamilika kwa michezo ya kimataifa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Mchezo huo namba 61 unatarajia kupigwa kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar es Salaam majira ya saa 11 jioni.
Taarifa kutoka bodi ya Ligi imeeleza kuwa mabadiliko hayo yametokana na baadhi ya nchi zimeendelea na kuweka masharti magumu katika taratibu za usafiri wa kimataifa tangu kuzuka kwa jana la ugonjwa wa Covid-19 jambo linazoweza kuathiri vikosi vya klabu zote mbili.
Michezo ya kimataifa inatarajia kuchezwa 10 mpaka 12 Oktoba, 2020 kutokana na kalenda ya Fifa ambapo Tanzania itacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Burundi.
Leave a comment