Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Sikukuu ya Eid yasherekewa kivingine Pugu
Habari Mchanganyiko

Sikukuu ya Eid yasherekewa kivingine Pugu

Wamama wa kiislamu wakishiriki mchezo wa mbio za magunia
Spread the love

VIJANA mbalimbali wa dini ya Kiislamu wamefanya michezo katika viwanja vya Pugu Kajiungeni jijini Dar es Salaam ili kuwasaidia kutojiingiza katika maovu inapofika siku za sikukuu, anaandika Faki Sosi.

Tamasha hilo la michezo ambalo liliwashirikisha vijana lilifanyika jana katika sherehe ya sikukuu ya Eid El Hajj, linalenga kuwaweka pamoja na hivyo kuwafanya wasiende disco na sehemu zingine za starehe.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana wa Kiislam, Yusuf Aboud ‘Babu Jongo’, amesema michezo iliyofanyika kwenye tamasha hilo ni pamoja na kukimbia kwa gunia, kukimbia na chupa kichwani na kuvuta kamba.

Aboud amewataka vijana wengi kujitokeza na kujiunga na Jumuiya hiyo kwa kuna mambo mengine wanaweza kufaidika nayo na siyo kuishia kufanya michezo pekee.

Jumuiya hiyo imefanikiwa kuimarisha maadili na amani kwa jamii katika eneo la Pugu na hiyo ni mara ya pili kufanyika tamasha hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!