Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Sikukuu ya Eid yasherekewa kivingine Pugu
Habari Mchanganyiko

Sikukuu ya Eid yasherekewa kivingine Pugu

Wamama wa kiislamu wakishiriki mchezo wa mbio za magunia
Spread the love

VIJANA mbalimbali wa dini ya Kiislamu wamefanya michezo katika viwanja vya Pugu Kajiungeni jijini Dar es Salaam ili kuwasaidia kutojiingiza katika maovu inapofika siku za sikukuu, anaandika Faki Sosi.

Tamasha hilo la michezo ambalo liliwashirikisha vijana lilifanyika jana katika sherehe ya sikukuu ya Eid El Hajj, linalenga kuwaweka pamoja na hivyo kuwafanya wasiende disco na sehemu zingine za starehe.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana wa Kiislam, Yusuf Aboud ‘Babu Jongo’, amesema michezo iliyofanyika kwenye tamasha hilo ni pamoja na kukimbia kwa gunia, kukimbia na chupa kichwani na kuvuta kamba.

Aboud amewataka vijana wengi kujitokeza na kujiunga na Jumuiya hiyo kwa kuna mambo mengine wanaweza kufaidika nayo na siyo kuishia kufanya michezo pekee.

Jumuiya hiyo imefanikiwa kuimarisha maadili na amani kwa jamii katika eneo la Pugu na hiyo ni mara ya pili kufanyika tamasha hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!