Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Freeman Mbowe afunguka uchaguzi Kenya
Makala & UchambuziTangulizi

Freeman Mbowe afunguka uchaguzi Kenya

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

MWENYEKITI  wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amefunguka na kumsifu Rais Uhuru Kenyatta kuwa mvumilivu na kuheshimu Wakenya baada ya kumalizika uchaguzi mkuu mwezi uliopita, anaandika Mwandishi wetu.

Mbowe amesema Kenyatta ameonyesha ukomavu kwa Marais wenzake wa Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla kwa kuwa aliruhusu kufanyika maandamano na kuamuru polisi kutoa ulinzi.

Akizungumza na kituo cha redio cha EATV leo asubuhi, Mbowe amesema Kenya wameonyesha ukomavu na vyombo vyao vya kutoa haki pia vimeonyesha kwamba vipo huru na haviingiliwi na mtu yoyote.

Amesema kitendo cha Mahakama ya Juu nchini humo kuamuru uchaguzi mkuu urudiwe hakinabudi kuigwa na nchi nyingi za Afrika.

Mbowe amesema katika kipindi chote tangu uchaguzi umalizike mwezi uliopita, Kenyatta amezidi kuonyesha ukomavu wa kisiasa na kwamba angeamua kutumia vyombo vya dola ambavyo vipo chini yake angeweza kuendelea kutawala lakini yeye hakutaka kufanya hivyo.

Mahakama ya Juu nchini Kenya jana ilifuta  ushindi wa rais Uhuru Kenyatta katika Uchaguzi uliofanyika tarehe 8 mwezi uliopita.

Uamuzi huo ulitangazwa na Jaji Mkuu David Maraga jijini Nairobi Ijumaa asubuhi. Jaji Maranga alisema kuwa kati ya Majaji sita waliosikiliza kesi hiyo, wanne walifikia uamuzi kuwa uchaguzi huo haukufanyika kwa mujibu wa Katiba ya sheria za Uchaguzi nchini humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & Uchambuzi

Ruth Zaipuna: Sekta ya kibenki imeimarika maradufu miaka miwili ya Dk. Samia

Spread the loveTarehe 19 ya mwezi Machi, ni siku muhimu sana kwa...

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Miaka miwili ya Rais Samia, TMA yaimarika, yatoa utabiri kwa usahihi

Spread the loveMACHI 19, 2023 Rais Samia Suluhu Hassan anatamiza miaka miwili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ampandisha cheo RPC wa Dar

Spread the loveMKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema...

Habari za SiasaTangulizi

Wanachama 384 CUF watimkia Chadema, Mbowe awapokea, Kambaya ndani…

Spread the loveJUMLA ya wanachama 384 wanachama wa Chama cha Wananchi CUF...

error: Content is protected !!