Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yataka majibu ya corona kwa saa 24
Habari Mchanganyiko

Serikali yataka majibu ya corona kwa saa 24

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imeagiza utoaji wa majibu ya vipimo vya ugonjwa wa corona ndani ya saa 24 badala ya saa 72. Anaandika Regina Mkonde…(endelea).

Akizungumza na Uongozi wa Maabara ya Taifa na Afya ya Jamii, Prof. Abel Makubi ambaye ni Mganga Mkuu wa Serikali leo tare he 26 Desemba 2020 amesema, hatua hiyo itaondoa malalamiko ya ucheleweshwaji kwa wale wanaotaka kusafiri.

Prof. Makubi amekutana na uongozi wa maabara hiyo, wasimamizi wa maabara na waganga wakuu kutoka hospitali za serikali na binafsi.

Ni baada ya kufanya ziara katika maabara hiyo kwa lengo la kusikiliza na kuangalia namna ya kutatua changamoto zinazokabili maabara hiyo.

“Ucheleweshaji wa majibu kamwe hauwezi kuvumiliwa,” amesema Prof. Makubi huku akisisitiza kuwepo malalamiko hayo hasa kutoka kwa wasafiri.

Ameutaka uongozi wa maabara hiyo kufanya lolote linalowezekana kuhakikisha wanatimiza la kutoa majibu ya vipimo vya corona ndani ya saa 24.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!