Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko OSHA kuwafikia wajasiriamali katika mazingira hatarishi
Habari Mchanganyiko

OSHA kuwafikia wajasiriamali katika mazingira hatarishi

Watengeneza batiki
Spread the love

WAKALA wa Usalama na Afya Mahala Pa Kazi (OSHA) umesema uko katika mkakati wa kuwafikia wajasiriamali, wanaofanya kazi katika mazingira hatarishi. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 2 Novemba 2019 jijini Dar es Salaam, Hadija Mwenda, Kaimu Mtendaji Mkuu OSHA, amesema wajasiriamali wengi wanafanya kazi katika mazingira hatarishi, kutokana na kutofikiwa na wakala huo.

Mwenda amesema OSHA ilishindwa kuwafikia wajasiriamali hao, kwa sababu ya kutosajiliwa, hali iliyosababishwa na kutokuwa na maeneo maalumu ya kufanyia kazi zao.

Kufuatia changamoto hiyo, Mwenda amesema OSHA imeanza utaratibu wa kuwafikia wajasiriamali hao, kwa lengo la kuwashauri namna ya kujikinga na mazingira hatarishi, kwenye mahala pa kazi.

Mwenda amesema hadi sasa OSHA imewafikia wajasiriamali 28,000 nchi nzima, na kwamba utaratibu huo ni endelevu ili kuhakikisha kundi hilo linafikiwa.

“Tuko kwenye mkakati wa namna ya kuwafikia wajasiriamali, sababu wanafanyakazi katika mazingira magumu na hatari. Mfano watengenezaji wa batiki hutumia kemikali hatari pasipo kuwa na elimu juu ya madhara yake na namna ya kujikinga,

Vvile vile mafundi gereji nao wako katika mazingira hatarishi. Hii yote ni kwa sababu hawajasiliwa. Inakuwa changamoto kuwajua walipo na namna ya kuwafikia,” amesema Mwenda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!