Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwijaku arudi uraiani
Habari Mchanganyiko

Mwijaku arudi uraiani

Burton Mwambe 'Mwijaku'
Spread the love

MSANII wa maigizo Burton Mwambe (35) maarufu kwa jina la Mwijaku, sasa amerejea uraiani baada ya kukaa siku tano mahabusu. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Mwijaku alipandishwa kzimbani kwa tuhuma za kusambaza picha za ngono kwenye mtandaoni, ambapo leo tarehe 3 Agosti 2020, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamucha kwa dhamana.

Awali, Mwijaku alipandishwa kizimbani tarehe 29 Julai 2020 na kusomewa shitaka la kusambaza picha za utupu kupitia mtandao wa Whatsapp.

Alisomewa shitaka hilo na Wakili wa Serikali, Mwanamina Kombakono mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Richard Kabate.

Mtuhumiwa huyo alikana mashtaka hayo ambapo Hakimu Kabate alimpa mashrati ya kuwa na wadhamini wawili watakaosaini bondi ya Sh. 500,000 kila mmoja.

Lakini pia wadhamini hao wote walitakiwa kuwa wasanii aidha wa filamu au muziki, wanaotambiliwa na Baraza la Sanaa (Basata) na kupewa baraka za baraza hilo.

Leo Mwijaku ameachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti alipewa na mahakama hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!