Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwanafunzi aliyetumbukia chooni aokolewa, Polisi kuchunguza
Habari MchanganyikoTangulizi

Mwanafunzi aliyetumbukia chooni aokolewa, Polisi kuchunguza

Spread the love

MWANAFUNZI wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Seliani iliyoko wilayani Arusha, Emanuel Zacharia amenusurika kifo baada ya kutumbukia katika shimo la choo cha shule hiyo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, SACP Ramadhan Ng’azi amethibitisha tukio hilo akisema kuwa, lilitokea asubuhi ya leo tarehe 26 Oktoba 2018, majira ya saa tatu na nusu asubuhi.

Akizungumza na mtandao huu, Kamanda Ng’azi ameeleza kuwa, Zacharia alipatwa na mkasa huo alipokwenda chooni kujisaidia, ambapo isivyo bahati shimo la choo lilitumbukia.

Ameeleza kuwa, baada ya tukio hilo kutokea, wananchi, waalimu na polisi walifanya jitihada za kumuokoa mwanafunzi huyo ambaye kwa sasa yuko katika Hospitali ya Seliani akipatiwa matibabu.

Kamanda Ng’azi amesema Jeshi la Polisi linachunguza chanzo cha tukio hilo, na kutoa saa tatu kwa uongozi wa shule hiyo kufanya marekebisho ya choo hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!