KIUNGO mshambuliaji wa Simba raia wa Ghana, Bernard Morrison amesema kuwa klabu ya Simba ndio chuo cha mpira wa miguu nchini Tanzania na hakuna klabu nyingine. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Mchezaji huyo ameyasema hayo wakati alipotambulishwa kwenye Tamasha la klabu hiyo maarufu kama ‘Simba Day’ lilofanyika kwenye Uwanja wa Mkapa, Jijini Dar es Salaam alipopewa nafasi ya kuongea na msemaji wa klabu hiyo Haji Manara mbele ya umati wa mashabiki wa Simba waliojitokeza huku akisema kuwa anaipenda sana timu hiyo.
“Naipenda Simba, kwani ndio chuo kikuu cha mpira wa miguu Tanzania na hakuna klabu nyingine,” alisema Morrison.
Mchezaji huyo ambaye amesajiliwa na klabu ya Simba akitokea Yanga baada ya mvutano wa muda mrefu na viongozi wa timu juu ya uhalali wa mkataba wake na baadae kamati ya Haki na Hadhi za Wachezaji kutoa uwamuzi ya mchezaji huyo kuwa huru baada ya kusikiliza shauli hilo.
Mchezaji huyo ambaye alikuja nchini January 2020 kujiunga na klabu ya Yanga kwa mkataba wa miezi sita na baadae kutimkia Simba ambapo amesaini makubaliano ya mkataba wa miaka miwili.
Hongera sana wana msimbazi kwa utendaji wenu
You’re right Morison, coz there is a college and university, for me i know that, there is no club in tnzania like simba more over we w’ll be cheating ourself.