Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge akumbuka wema wa Mkapa
Habari za Siasa

Mbunge akumbuka wema wa Mkapa

Njalu Daudi, Mbunge aliyemaliza muda wake wa Itilima Mkoa wa Simiyu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwa na Hayati Benjami Mkapa
Spread the love

MBUNGE aliyemaliza muda wake wa Itilima Mkoa wa Simiyu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Njalu Daudi amesema, wananchi wa jimbo hilo watamkumbika Hayati Rais mstaafu wa Tanzania, Benjamini William Mkapa kwa mchango wake kwenye sekta ya afya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Simiyu … (endelea).

Mkapa amefariki dunia Alhamisi tarehe 23 Julai 2020 katika moja ya hospitali jijini Dar es Salaam kwa tatizo la mshituko wa moyo na mwili wake utazikwa Jumatano tarehe 29 Julai 2020.

Daudi ambaye ameongoza kura za maoni kutetea nafasi hiyo katika Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020, amesema Hayati Mkapa alikuwa mzalendo wa kweli kwa Taifa na Afrika.

Amsema enzi za uhai wa Mkapa aliyeongoza Tanzania kwa miaka kumi mfululizo kuanzia mwaka 1995 hadi 2005 aliwasaidia kujenga jengo la upasuaji kupitia Taasisi ya Mkapa Foundation katika kata ya Nkoma.

“Alikua ni rafiki yangu, taifa limepoteza shujaa wa nchi na nguzo ya Afrika, tumuombee apumzike kwa amani,” amesema Daudi.

“Aidha kwetu katika kata ya Nkoma, tulikua na tatizo la kutokua na chumba cha upasuaji, Mkapa alihakikisha kupitia Mkapa Foundation anatimiza ndoto za wananchi wengi waishio Nkoma.”

“Sasa wazazi na wananchi wanapata huduma zote vyema na katika sehemu salama, alitumia zaidi ya Sh.270 million na kwa kweli ameacha alama maishani mwetu,‘’ amesema Silanga

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!