Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe aendesha kikao cha kamati kuu kidigitali
Habari za Siasa

Mbowe aendesha kikao cha kamati kuu kidigitali

Spread the love

KAMATI Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imeanza vikao vyake leo Jumamosi tarehe 9 Mei 2020 kwa njia ya kidigitali chini ya Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa iliyotolewa kwa umma na Tumaini Makene, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Chadema imesema vikao hivyo vitajadili masuala mbalimbali ikiwamo janga la mlipuko wa ugonjwa wa COVID-19 na hali ya kisiasa.

Makene amesema maazimio kuhusu agenda hizo yatatolewa baada ya vikao kukamilika.

Amesema Chadema imeamua kufanya vikao vyake kwa njia ya mtandao ili kusaidia wahusija kujikinga dhidi ya corona.

“Kufanyika kwa mfululizo kwa vikao hivi kwa njia ya mtandao, Chadema imetekeleza kwa vitendo ushauri iliyotoa kwa serikali na bunge katika kuchukua tahadhari ya kupunguza mikusanyiko, katika kuendesha shughuli zake, ili kusaidia wahusika kujikinga dhidi ya ugonjwa wa Covid-19,” amesema Makene.

Kikao hiko kinafanyika kipindi ambacho kumeahuhudi baadhi ya wabunge wake wakikaidi maagizo yakiyotoleaa tarehe 1 Mei 2020 ya kujitenga kwa siku 14 kwa kutofanya shughuli zozote za kibunge.

Maagizo hayo yaliyolewa na Mbowe ambaye ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni baada ya vifo vya wabunge na wananchi aliodai vimetokana na corona hivyo kujitenga kwa siku 14 kwa kukaa majumbani mwao kunaweza kusaidia kutambua afya zao.

Hata hivyo, zaidi ua wabunge 12 walikaidi maagizo hayo na wamekuwa wakihudhuria vikao vya Bunge kama kawaida huku Spika wa Bunge, Job Ndugai akiwaonya wale wote wanaoendelea kukaa nyumbani kwani watahesabiwa kama watoro.

Duru za siasa zinaonyesha huwenda miongoni mwa maadhimio ya kikao hicho cha kamati kuu ikawa na kuwachukulia hatua zaidi za kinidhamu wabunge hao waliokaidi.

Tayari wabunge hao wamekwisha kuondolewa katika kundi la wabunge la WhtasApp.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!