Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Manara achomoka sakata la MO
Habari Mchanganyiko

Manara achomoka sakata la MO

Haji Manara
Spread the love

MKUU wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Haji Manara pamoja na watu 19 waliokuwa wanashikiliwa kutokana na sakata la kutekwa kwa Mfanyabishara Mohammed Dewji ‘Mo Dewji’,  wamechwa huru kwa dhamana. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa inaeleza kuwa Manara na wenzake wameachwa kwa dhamana usiku wa jana tarehe 15 Oktoba 2018.

Manara aliyesota rumande tangu Oktoba 12 mwaka huu hadi usiku wa jana, alikamatwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kusambaza taarifa za tukio la kutekwa kwa Mo Dewji akidai alitumwa na familia ya mfanyabiashara huyo, wakati si kweli.

Katika sakata hilo, watu 7 kati ya 26 akiwemo Manara na wenzake 19 walioachwa huru kwa dhamana, bado wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam wakihusishwa na tukio la Kutekwa kwa Mo Dewji lilitokea katika hoteli ya Colosseum jijini Dar es Salaam Oktoba 11 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!