Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Manara achomoka sakata la MO
Habari Mchanganyiko

Manara achomoka sakata la MO

Haji Manara
Spread the love

MKUU wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Haji Manara pamoja na watu 19 waliokuwa wanashikiliwa kutokana na sakata la kutekwa kwa Mfanyabishara Mohammed Dewji ‘Mo Dewji’,  wamechwa huru kwa dhamana. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa inaeleza kuwa Manara na wenzake wameachwa kwa dhamana usiku wa jana tarehe 15 Oktoba 2018.

Manara aliyesota rumande tangu Oktoba 12 mwaka huu hadi usiku wa jana, alikamatwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kusambaza taarifa za tukio la kutekwa kwa Mo Dewji akidai alitumwa na familia ya mfanyabiashara huyo, wakati si kweli.

Katika sakata hilo, watu 7 kati ya 26 akiwemo Manara na wenzake 19 walioachwa huru kwa dhamana, bado wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam wakihusishwa na tukio la Kutekwa kwa Mo Dewji lilitokea katika hoteli ya Colosseum jijini Dar es Salaam Oktoba 11 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!