Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli nusura awatumbue DED, DC mkutanoni
Habari za Siasa

Magufuli nusura awatumbue DED, DC mkutanoni

Rais John Magufuli, mgomba Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM
Spread the love

JOHN Mwaipopo, Mkuu wa Wilaya ya Igunga (DC) na Revocatus Kuuli, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya hiyo (DED) mkoani Tabora, nusura watumbuliwe. Anaripoti Mwandishi Wetu, Igunga … (endelea).

Ni baada ya Rais John Magufuli ambaye ni mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuagiza viongozi hao kuacha tofauti zao na kwamba, anajua vizuri mgogoro unaofukuta miongoni mwao.

Ametoa agizo hilo wakati akizungumza katika mkutano wa kampeni za urais za chama hicho leo Jumatano tarehe 2 Septemba 2020, wilayani Igunga mkoani humo.

“Ninafahamu hapa baadhi ya watendaji wangu nataka mjirekebishe, Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri ya hapa, mimi napendaga kusema ukweli na msema ukweli mpenzi wa Mungu,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ambaye ni ngombea urais wa Tanzania kupitia chama hicho, amemuagiza Kuuli kurudisha madeni anayodaiwa sambamba na kutatua changamoto za ardhi.

“Mkurugenzi aliko kule arudishe madeni yote anayodaiwa, atatue matatizo ya ardhi. Anachukua mpaka maeneo ya watu, hizi ndizo salamu zake mumpelekee,” amesema Rais Magufuli.

Rais huyo wa Tanzania amesema, wananchi wanapata mateso kutokana na kukosa watu wa kufikisha changamoto zao katika mamlaka husika.

“Mateso mengine mnayoyapata mlitakiwa mpate watu wa kuwasemea sababu hayafiki mahali inapotakiwa,” amesema Rais Magufuli.

Kuhusu Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Rais Magufuli amesema mteule wake huyo aliwahi kumfukuza mwananchi aliyempelekea taarifa za kutishiwa usalama wa maisha yake badala ya kumsaidia.

“Kuna mtu mmoja alishinda kesi ya dhuruma zao kule baadae akawa anatishiwa kuuawa akaenda kwa mkuu wa wilaya kueleza alitishiwa kuuawa, mkuu wa wilaya akamfukuza baada ya siku mbili yule mtu akauawa, nasema uongoz ndugu zangu?” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!