JESHI la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani limewafutia leseni za udereva wadereva watatu na kuwafungia milele kuendesha magari aina ya mabasi pamoja na yale ya mizigo kwa kosa la kusababisha ajali na vifo, anaandika Faki Sosi.
Kadhalika, madereva saba wamefutiwa leseni zao za daraja ‘C’ na ‘E’ kwa makosa ya kuendesha kwa kasi zaidi ya kilometa 90 kwa saa.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Kamanda wa Kikosi hicho Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Fortunatus Musilimu amesema madereva hao hawaturuhusiwa kuendesha gari za abiria au mizigo kwa muda wa miezi sita.
Musilimu amesema madereva hao wanatakiwa kurudi darasani, kusoma upya na kupewa mitihani na kama watafaulu watapewa leseni upya.
Amewataja madereva hao kuwa Hamadi Salumu mwenye Leseni namba 4001852854, Kija Mayenga (4001518000), Issack Mbijina (4000220395), Hassan Semazua (4001522366), Stanley Mosha (4000369436).
Wengine Abdallah Husseni (4000482412) ambaye hadi sasa yupo mahabusu kwa kushindwa kulipa fainin na Sempunda Yusufu (1-1980,80006518226).
Madereva waliofungiwa kuendesha magari milele ni pamoja na Ismail Nyami, mwenye leseni 4000676285 ambaye alisababisha ajali Septemba 23, mwaka huu iliyoua watu wawili, na kujerehi 42 wilayani Nyasa mkoani Ruvuma, na Mseka Salumu, (4000118648) aliyesababisha ajali Septemba 25 mwaka huu iliyoua mtu mmoja na kujeruhi 25 eneo la Maganzo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga
Mwengine ni Malik Hassani (4000450337) aliyesababisha ajali Septemba 21 mwaka huu na kuua mtu mmoja na kujeruhi sita.
Leave a comment