Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mabomu yarindima Segerea ‘kwa Mbowe’
Habari za Siasa

Mabomu yarindima Segerea ‘kwa Mbowe’

Spread the love

ASKARI wa Jeshi la Magereza katika gereza la Segerea, wametumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), walikwenda kumsubiri Freeman Mbowe nje ya lango la gereza hilo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Nguvu hiyo ilitumika baada viongozi na baadhi ya wanachama wa Chadema kufika katika gereza hilo, ili kukamilisha taratibu za kumtoa Mbowe.

Viongozi hao wa Chadema walikwenda Segerea baada ya kukamilisha masharti ya faini ya Sh. 70,000,000, hata hivyo walipofika getini, askari hao waliwazuia kuingia.

Kutokana na kuzuiwa, Halima Mdee, Mbunge wa Kawe na viongozi wengine waliokwenda, walishuka kwenye gari ili kusikilizana na askari hao.

Hivyo, wafuasi wa chama hicho waliokuwa eneo hilo, nao walisogea kusikiliza na kushinikiza viongozi wa Chadema waachwe kwenda kukamilisha taratibu za kumtoa Mbowe.

Askari hao walianza kuwapiga na kukamata baadhi ya wafuasi hao, na walipoona hali inazidi kuchafuka, wakalazimika kutumia mabomu ya machozi jambo lililozua taharuki eneo hilo.

Mmmoja kati ya wafuasi alalamika, kuwa licha ya kukamilisha masharti ya kumtoa Mbowe gerezani, bado mamlaka ya gereza hilo inajizungusha kumtoa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!